![]() |
![]() |
MATAKASO
KABLA YA KUAHIDI MASHAURI YA KIINJILI
TAKASO LA KWANZA YAANI TAKASO LA MATOWASHI
219. Siku ya kawaida ya wakati wa matakaso ya watakaoweka ahadi, jamaa inawakusanyikia kwa ibada muhimu ya takaso la kwanza, ambalo linahusiana na shauri la Kiinjili la useja mtakatifu na kulenga kuwaimarisha dhidi ya vishawishi, kunyosha nia zao, kuchochea utashi wao, kuongeza ujuzi mnyofu na mnyenyekevu wa nafsi yao kwa njia ya kujitafiti na kutubu kwa dhati. Hivyo wanaandaliwa kushika vema ahadi hiyo na madai yake. Inafaa kuadhimisha ibada hii katika kikanisa cha jumuia ya zoezi baada ya Zaburi za Sala ya Mchana ikihudhuriwa na wanajumuia tu.
220. Kama kawaida, katika ibada ina nafasi ya msingi Liturujia ya Neno, ambayo inapendekezewa masomo mbalimbali ya kuchagua (taz. namba 379) lakini moja tu kutoka Injili, kwa kuwa ni la lazima na ndilo linalolipa takaso jina lake.
221. Baada ya hotuba, watakaoweka ahadi wanajipanga mstarini mbele ya padri ambaye, kwanza anawaelekea ndugu waliopo awaalike kuwaombea kimya roho ya toba, hofu ya dhambi na ukombozi kamili wa miili yao. Halafu anawaalika wenyewe kusali kimya wakitokeza msimamo wao wa ndani wa toba na kujiombea neema kwa kupiga magoti.
222. Baada ya kimya kidogo, padri anawaalika waote kusali pamoja kwa maneno ya namna hii:
223. Shemasi anatoa nia za namna hii:
Ili
wakiri kwa unyenyekevu ukosefu wao na kurekebisha maisha yao mbele ya Yesu
aliyekuja kuokoa waliopotea, tuombe:
Ili
waepukane na hali ya kukata tamaa, inayosogeza mbali na njia ya Kristo, tuombe:
Ili
kwa msimamo wao mnyofu wayakatae siku kwa siku katika mwenendo wao yale yote
ambayo hayampendezi Baba bali yanapingana na sheria yake ya upendo, tuombe:
Ili
Roho Mtakatifu anayechunguza mioyo ya wote autegemeze udhaifu wao kwa uweza
wake, tuombe:
Ili
sisi pia, tukijiandaa kushuhudia ahadi zao, tutakase mioyo yetu isipende kwa
namna yoyote dhambi na nyinginezo zinazopingana na utakatifu wa wito wetu,
tuombe:
Ili
katika ulimwengu wote, yaliyo dhaifu yaimarishwe, yaliyoanguka yainuliwe,
yaliyooza yaponywe, na hivyo viumbe vyote vishirikishwe ushindi wa Pasaka,
tuombe:
224. Halafu padri, akiwaelekea watakaoweka ahadi anasali amefumba mikono:
Mwenyezi
Mungu, uliye mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu,
unapendelea
roho zisizo na doa
na
kutamani kukaa mwilini mwa walio safi kama hekaluni mwako,
ulivyozoea
kufanya katika Mwanao mpenzi Yesu Kristo.
Kwa
njia yake na kwa ajili yake uliumba ulimwengu
nasi
watu kwa sura yake upande wa mwili
na
kwa mfano wake upande wa roho.
Ulipoamua
kurekebisha upya maumbile ya binadamu,
yaliyoharibiwa
na hila za Ibilisi tangu wazazi wetu wa kwanza,
hukuridhika
kuyarudishia utakatifu asili tu,
bali
kwa stahili za Neno wako aliyefanyika mwili,
umewainua
watu wafanane na malaika,
ukiwawezesha
kutanguliza ndani mwao hali ya ufalme ujao
ambapo
hawataoa wala kuolewa, bali upendo utawaenea wote.
Uwaongoze
daima wateule hawa,
ambao
kwa mwanga wa hekima ya milele
umewajalia
kuelewa jinsi useja mtakatifu ulivyo bora
na
kuwa chemchemi halisi ya karama hiyo ni wewe tu.
Kwa
maana roho yenye mwili unaoelekea uharibifu,
inawezaje
kushinda silika ya maumbile, upotovu wa hiari,
mitikisiko
ya hisi na misukumo ya umri,
isipokuwa
kwa sababu wewe, Baba wa rehema,
umewasha
na kuchochea ndani mwake moto wa upendo wako,
na
kuishirikisha nguvu zako mwenyewe?
Tunakuomba
hayo kwa njia ya Kristo, Bwana wetu.
225. Wote wanaitikia:
Amina.
226. Padri anamwekea mikono kichwani kila mmoja wa watakaoweka ahadi, halafu, akiwanyoshea wote pamoja, anaendelea na sala:
Bwana
Yesu, ulilipenda Kanisa ukajitoa kwa ajili yake,
nawe
unazidi kulitakasa na kulifanya upya
ulilete
mbele yako kama bikira asiye na doa,
kama
mchumba aliyepambwa kwa ajili ya arusi,
kama
mama anayefurahia wingi wa watoto
wasiozaliwa
kwa mwili tu, bali kwa Roho Mtakatifu.
usikubali
wadanganywe na yule mwovu
wala
kujiamini kipumbavu,
bali
waoanishe adabu na uangalifu, wema na busara,
227. Wote wanaitikia:
Amina.
228. Kipindi kinamalizika kama kawaida kwa baraka au kwa shangilio:
Tumtukuze Bwana.
Tumshukuru Mungu.
TAKASO LA PILI YAANI TAKASO LA WENYE HERI
229. Baada ya mwezi mmoja hivi, linafanyika takaso la pili linalohusiana na shauri la Kiinjili la ufukara wa hiari ambao mzee wetu Fransisko ametufundisha kuukumbatia sana kama ufukara mkuu. Kimsingi, taratibu na malengo ya ibada hii ni kama vile vya takaso la kwanza. Inafaa kuifanya siku ya kawaida katika kikanisa cha nyumba ya zoezi baada ya Zaburi za Sala ya Mchana, ikihudhuriwa na wanajumuia tu.
230. Kama kawaida, katika ibada ina nafasi ya msingi Liturujia ya Neno, ambayo inapendekezewa masomo mbalimbali ya kuchagua (taz. namba 380) lakini moja tu kutoka Injili, kwa kuwa ni la lazima na ndilo linalolipa takaso jina lake.
231. Baada ya hotuba, watakaoweka ahadi wanajipanga mstarini mbele ya padri ambaye, kwanza anawaelekea ndugu waliopo awaalike kuwaombea kimya roho ya kulenga mema ya milele badala ya mali, hamu ya kuwa wadogo na kudharauliwa kwa upendo wa Yesu fukara na wa wale wote wanaobaguliwa badala ya kuwa wakuu. Halafu anawaalika wenyewe kusali kimya wakitokeza msimamo wao wa ndani wa toba na kujiombea neema kwa kupiga magoti.
232. Baada ya kimya kidogo, padri anawaalika waote kusali pamoja kwa maneno ya namna hii:
Tuwaombee tena ndugu hawa,
wanaoelekezwa kufuata nyayo za Kristo katika utawa wetu, ili waambatane na
ufukara wake kwa moyo wote, wakikubali yale yote yanayotokana nao.
233. Shemasi anatoa nia za namna hii:
Ili wateule hawa watafakari sana
hekima ya msalaba, ambayo Mungu anaaibisha ile ya ulimwengu, tuombe:
Ili wadumu kuwa waaminifu kwa roho ya
Kiinjili ya udugu na mshikamano, unyofu na furaha, hata ulimwengu utakapojaribu
kuwameza, tuombe:
Ili katika maisha ya wateule hawa,
watu maskini na wenye njaa, wanaobaguliwa na kudhulumiwa, waone thibitisho la
heri yao, tuombe:
Ili sisi sote tunuie tena kufuata
ufukara wa Kiinjili hata tushuhudie unavyoleta uhuru wa moyo, tuombe:
Ili Kanisa, likisafiri hapa duniani
kati ya udhia za ulimwengu na faraja za Mungu, limfuate kabisa Bwanarusi wake na
kuifanya roho ya ufukara na ya upendo iwe ndiyo fahari yake, tuombe:
Ili ulimwengu mzima uache kudanganywa
na miungu yote ya uongo na upate ukombozi kamili katika Kristo na katika Kanisa
lake, tuombe:
234. Halafu padri, akiwaelekea watakaoweka ahadi anasali amefumba mikono:
Lo,
ufukara wa Kimungu!
Bwana
wetu Yesu Kristo,
ambaye
akisema vyote vinafanyika,
aliukumbatia
kuliko yote,
akikosa
hata mahali pa kulaza kichwa chake,
mpaka
akakiinamisha atutolee Roho wake!
Ufukara
wenye heri unaowashirikisha mema ya milele
wale
wanaoupenda!
Ufukara
mtakatifu ambao walionao na wanaoutamani
uliwaahidia
ufalme wa mbinguni
na
kuwatolea utukufu na uzima usio na mwisho!
235. Wote wanaitikia:
Amina.
236. Padri anamwekea mikono kichwani kila mmoja wa watakaoweka ahadi, halafu, akiwanyoshea wote pamoja, anaendelea na sala:
ili
utwae mwili na kukaa kwetu
kwa
nguvu ya Roho Mtakatifu,
ukawatangazia
maskini habari njema ya ukombozi kamili;
ukawaweka
wawe mitume wako Wagalilaya duni,
waliofahamu
ukosefu wao,
na
waliokuwa tayari kuacha vyote kwa ajili yako.
Ummimine
tena Roho Mtakatifu juu ya wateule hawa
wasadiki
kweli na kuonja heri uliyoitangaza kwanza,
kwa
kushika ufukara mkuu wa Injili yako.
Wawe
wanyenyekevu na wanyofu,
wamtii
mtu yeyote kwa ajili yako,
wajichukie
na kuwapenda wanaowapiga shavu,
wapokee
siku kwa siku riziki zao,
na
kushirikisha kwa ukarimu kilichopatikana.
Wavihesabu
vyote kuwa ni takataka ili wakupate wewe
ambaye
kwa upendo wao ulijinyima hata pa kupumzikia,
ukaufanya
msalaba tupu uwe ndio kiti chako cha enzi.
Wakukazie
macho wewe,
uliyeanzisha
na kutimiliza imani yetu,
wakijihadhari
na mashauri ya kibinadamu tu,
wasije
wakaacha kwa namna yoyote nyayo zako,
wala
wasiangalie nyuma baada ya kushika jembe,
wala
wasiache katikati ujenzi waliouanza,
kama
mpumbavu asiyejua sharti la kuacha vyote
ili
kukufuata hadi kikomo cha safari ya upendo,
kufa
uchi msalabani ulivyofanya wewe,
unayeishi na kutawala daima na milele.
238. Kipindi kinamalizika kama kawaida kwa baraka au kwa shangilio:
Tumtukuze Bwana.
Tumshukuru Mungu.
TAKASO LA TATU YAANI TAKASO LA NDUGU
239. Baada ya mwezi mmoja hivi, linafanyika takaso la tatu linalohusiana na shauri la Kiinjili la utiifu wa kitawa ambao pia mzee wetu Fransisko ametusisitizia sana akiuweka kama mpaka dhambi tu. Kimsingi, taratibu na malengo ya ibada hii ni kama vile vya matakaso yaliyotangulia. Inafaa kuifanya siku ya kawaida katika kikanisa cha nyumba ya zoezi baada ya Zaburi za Sala ya Mchana, ikihudhuriwa na wanajumuia tu.
240. Kama kawaida, katika ibada ina nafasi ya msingi Liturujia ya Neno, ambayo inapendekezewa masomo mbalimbali ya kuchagua (taz. namba 381) lakini moja tu kutoka Injili, kwa kuwa ni la lazima na ndilo linalolipa takaso jina lake.
241. Baada ya hotuba, watakaoweka ahadi wanajipanga mstarini mbele ya padri ambaye, kwanza anawaelekea ndugu waliopo awaalike kuwaombea kimya roho ya kujikana kabisa, hadi kujikatalia maoni na matakwa kadiri yanavyopingana na yale ya Mungu. Halafu anawaalika wenyewe kusali kimya wakitokeza msimamo wao wa ndani wa toba na kujiombea neema kwa kupiga magoti.
242. Baada ya kimya kidogo, padri anawaalika waote kusali pamoja kwa maneno ya namna hii:
243. Shemasi anatoa nia za namna hii:
Ili
wateule hawa wazidi kuungana na Baba kwa njia ya utiifu mtakatifu,
tuombe:
Ili
wamfuate Yesu, aliyejifunza kwa njia ya mateso kutii, na hivyo wakamilishwe
pamoja naye, tuombe:
Ili
Roho Mtakatifu awasaidie kutambua zaidi na zaidi matakwa ya Mungu, yaliyo mema,
ya kumpendeza na makamilifu, tuombe:
Ili
wajue namna ya kuwajibika, wakishirikiana na watumishi na walinzi katika
utambuzi huo, tuombe:
Ili
sisi sote tuchunguze upya msimamo wetu wa ndani kuhusu uongozi wa Mungu katika
maisha yetu, na hasa imani yetu, iliyo msingi wa utiifu, tuombe:
244. Halafu padri, akiwaelekea watakaoweka ahadi anasali amefumba mikono:
Baba
Mtakatifu sana,
umependa
Mwanao mbarikiwa na mtukufu
ajitoe
mhanga juu ya altare ya msalaba
kama
sadaka hai ya kufidia uasi wetu.
Hivyo
alituachia mfano tufuate nyayo zake
kwa
kuweka mapenzi yako matakatifu juu ya yote,
yawe
chakula cha kwanza kwa ustawi wa uhai wetu.
kupokewa
kwenye utiifu ndani ya utawa wetu:
uwafumbue
macho ya imani ili,
wakikutolea
sadaka kile kilicho muhimu zaidi kwao, yaani hiari,
watambue
kutii si swala la nidhamu tu,
bali
ni njia ya hakika ya ukamilifu
ambayo
wewe, mchungaji wao,
unawaelekeza
nukta baada ya nukta.
Watambue
pia kizuio kikuu cha utakatifu na wokovu,
yaani
kujitwalia utashi wao kama alivyofanya Adamu,
na
kujitukuza kwa mema yale
ambayo
mwenyewe unaonyesha na kutenda ndani mwao.
Kwa
hiyo wajikane kabisa
na
kujitia mikononi mwa viongozi wa Kanisa na wa utawa,
wasimtazame
mtu tu, uliyemshirikisha mamlaka yako,
ila
ndani mwake wakuheshimu wewe
ambaye
wamejiweka chini yake kwa upendo wako.
Uwajalie
wasijisingizie kwamba wanataka kufuata mambo mema
kuliko
yale waliyoagizwa,
wala
wasirudie matapishi ya matakwa yao
hata
kukwaza na kuua roho nyingi.
Uwatie
nguvu za kutekeleza unayoyaagiza,
halafu
uwaagize yoyote yale unayoyataka.
Kwa njia ya Kristo Bwana wetu.
245. Wote wanaitikia:
Amina.
246. Padri anamwekea mikono kichwani kila mmoja wa watakaoweka ahadi, halafu, akiwanyoshea wote pamoja, anaendelea na sala:
Bwana
Yesu Kristo,
uliwapenda
watoza ushuru na makahaba
kuliko
wanaokataa kufuata njia ya Mungu
wajiundie
sura ya kuwapendeza.
Ulitia
matakwa yako katika matakwa ya Baba
hata
kufa, naam, hata kufa msalabani,
ukatualika
tubebe siku kwa siku
mzigo
unaoufanya kuwa mwepesi,
tukitekeleza
mfululizo wajibu wetu
na
kumtii kabisa Baba
kama
watoto wanyenyekevu wenye upendo
ili
tuwe kweli wadogo wako.
Uwajalie
wateule hawa watambue na kuonja
jinsi
ilivyo tukufu, takatifu na kuu
kuwa
na Baba mbinguni ambaye wafanye kazi zake;
jinsi
ilivyo takatifu, nzuri na tamu kuwa na Bwanaarusi mbinguni
ambaye
waungane naye katika nia moja.
Wasiwe
wapumbavu kiasi cha kujifanyia mipango,
bali
wawe daima macho kutambua na kutekeleza ule wa Baba,
ambao
ni bora hata ukileta uchungu mwingi.
Wasisogee
mbali na maagizo yake, yawe ni wazi au la,
wala
wasizurure nje ya utiifu,
bali
wapendelee kuagizwa kuliko kuruhusiwa
na
zaidi tena kuitikia wito wa kimisionari utokao kwake.
Kwa
njia ya utiifu mtakatifu washinde
matakwa
yote ya kibinadamu tu,
wakiweka
mwili chini ya roho,
na
utu mzima chini ya watu na viumbe
kadiri
Baba atakavyopenda.
Wasitamani
kukaa juu ya wenzao,
bali
waamini kuwa aliyekubali nira ya wengine
hakuna
nukta inayopotea bure kwake,
tena
kuwa unyenyekevu wa yule anayetii kikamilifu kwa furaha
ni
mkubwa kadiri alivyo duni yule aliyetoa agizo.
Kwa
njia hiyo wajipatie uhuru wa wana wa Mungu,
wasiwe
watumwa wa machaguo ya ubinafsi na ya ukaidi,
wa
shaka, wasiwasi na fadhaiko,
wala
wasifuate fikra za kidunia, mitindo ya ulimwengu na mabishano;
hatimaye
wawe tayari kupenda na kutumikia tu
bila
ya kujitafutia faida yoyote, isipokuwa wewe
unayeishi
na kutawala daima na milele.
247. Wote wanaitikia:
Amina.
248. Kipindi kinamalizika kama kawaida kwa baraka au kwa shangilio:
Tumtukuze Bwana.
Tumshukuru Mungu.