Ndugu Wadogo Wa Afrika

Jina  
NDUGU

Umoja wa kidugu ni mang’amuzi matamu lakini ya nadra:

unawezeshwa tu na upendo ule ambao Yesu aliuishi mpaka mwisho

akatushirikisha katika Roho wake.

Ni jambo la kutekelezwa kwa wote na katika ngazi zote,

katika hali halisi ya maisha ya kila siku,

kwa furaha ya Baba yetu sote.  

WADOGO  

Hata katika ulimwengu wa G8,

wa wenye uwezo wanaofanya lolote wanalotaka,

inawezekana kujichagulia maisha ya wadogo, kama alivyofanya Fransisko wa Asizi.

Kwa sababu kilicho kidogo ni kizuri,

kwa kuwa Mungu amejifanya mdogo,

ili kusimama upande wa watu wa mwisho,

na kushikamana na wale wanaoshindwa katika ushindani wa kimataifa.  

WA AFRIKA  

Bara asili la binadamu wote,

labda kwa sababu hiyo linavutia kuliko yote.

Ni nchi ya watu wanaodhulumiwa tangu zamani,

wenye tunu nyingi za kiutu za kuweza kushirikisha,

lakini wametupwa pembeni kwa historia na uchumi wa kimataifa.

Limegeuzwa kuwa jalala isiyo na mipaka,

mgodi wa kushindaniwa,

soko kubwa la kuuzia bidhaa.  

Lebo   

Chama, kilichoanza wakati wa upapa wa Yohane Paulo II, kinafuata Kanuni aliyowathibitishia ndugu wa kiume na wa kike wa Utawa Hasa wa Tatu wa mtakatifu Fransisko.

 

Zaidi ya hayo, kimechota kwa wingi katika maisha yake ya Kiroho yaliyozama ndani ya fumbo la Kristo na Maria na kujitokeza katika ngao yake ya kipapa yenye herufi M (yaani Maria) chini ya msalaba.

 

Kwa hiyo wanachama wanavaa saa zote kanzu ya Kifransisko ambayo upande wa moyo ina lebo inayotumia ishara hizohizo juu ya ramani nyeusi ya Afrika.

 

Bara hilo, ambalo pengine lina hali ngumu kiasi cha kutisha, linatawaliwa tayari tena italibidi lizidi kutawaliwa na msalaba wa Kristo, mwekundu kwa damu na kama moto wa Upendo wa Mungu unaotakiwa kupamba duniani kote.

 

Chini yake, M nyeupe linamaanisha moyo safi wa Maria, uliomwezesha kutazama kwa dhati na kushiriki kikamilifu mpango wa Mungu ulipotimia katika sadaka ya utiifu wa Mwanae kwa wokovu wa binadamu wote.

 

Lebo ni mwaliko na hamu ya kuwa wana halisi wa Maria, wenye moyo safi wa kimama kama wa kwake mbele ya msalaba wowote ambao Yesu anaendelea kuteseka ndani ya wale aliowaita ndugu zake wadogo, akitangaza kwamba mwishoni tutahukumiwa kuhusu yale yote ambayo tumemtendea au kuacha kumtendea kila mmojawao.  

 

LINKS:

 

WIMBO WA TAIFA

Mungu Ibariki Afrika

Wabariki viongozi wake

Hekima, umoja na amani

Hizi ni ngao zetu

Afrika na watu wake. 

CHORUS:    

Ibariki, Afrika

Ibariki, Afrika

Tubariki, watoto wa Afrika

Morogoro, 9 luglio 2000: L’Associazione in festa attorno ai 5 nuovi professi perpetui - Morogoro, 9 Julai 2000: Utawa ukishangilia ndugu 5 walioweka ahadi ya daima - Morogoro, July 9th 2000: The Association celebrates the perpetual promises of five brothers and sisters