Alfagems Co. ltd

Secondary School

Morogoro Tanzania

Nafasi za Masomo

 

                       JIMBO KATOLIKI LA MOROGORO                                                                                   

ALFAGEMS SECONDARY SCHOOL (S.3874)

S.L.P. 6083 – MOROGORO

Tel. 0732-931605 (Ofisi) / 0789-978886 (Airtel Money)

0655-425723 (kuwasiliana Tigo Pesa) / 33708 (uwakala wetu Tigo Pesa)

0752-452444 (kuwasiliana M-Pesa) / 237405 (uwakala wetu M-Pesa)

0714-176745 (Bweni la kiume la chini) / 0786-906311 (Bweni la kiume la juu)

www.alfagems.com

 

 

Casella di testo: NAFASI ZA MASOMO

 

 

Ø  Shule yetu inazingatia taaluma na maadili kwa kufuata sera ya elimu ya Kanisa Katoliki.

Ø  Tunawashukuru nyinyi, wananchi wote, kwa kuonyesha mmeipenda sana.

Ø  Tunasikitika kulazimika kupandisha ada kutokana na ongezeko la mishahara na mfumuko wa bei.

Ø  Sababu nyingine ni kwamba tangu mwaka 2009 tunazidi kuomba ruzuku ya serikali lakini bado.

Ø  Kumbe tumeongezewa kodi (SDL) isiyozingatia mapato bali matumizi (5% ya mishahara yote): hivyo pesa zote za fomu zitapelekwa serikalini kulipia kodi hiyo.

Ø  Pamoja na kuwaahidia juhudi endelevu za kuboresha huduma, tunawatangazia nafasi zifuatazo.

Ø  Tafadhali, kabla hamjanunua fomu, ulizeni vizuri kuhusu masomo yanayowafaa zaidi.

Ø  Baadaye hamtaruhusiwa kubadili fomu wala masomo, kwa sababu ni lazima twende kwa mpango.

 

 

MASOMO YA SEKONDARI KUANZIA ASUBUHI

Ni elimu rasmi kwa wale tu wenye sifa za kufanya mitihani ya taifa kama wanafunzi wa shule; wengine wafikirie masomo ya jioni.

 

F I: KUINGIA KIDATO CHA KWANZA (Civics, History, Geography, English, Kiswahili, Biology, Chemistry, Physics, Mathematics na Information & Computer Studies). Wanaotaka kujiunga wawe wamezaliwa si kabla ya mwaka 1998 na kufaulu mtihani wa darasa la saba mwaka 2013 au 2014. Usaili utafanyika tarehe 15-11-2014 na 22-11-2014 saa 2:00 asubuhi. Washindi wataanza masomo tarehe 1-12-2014. Ada ni Tsh. 360,000 kwa mwaka. Kwa kukaa bweni wataongeza Tsh. 500,000. Jumla ni Tsh. 860,000.

 

F V: KUINGIA KIDATO CHA TANO (History, Kiswahili na Language; au History, Geography na Kiswahili; au History, Geography na Language; au History, Geography na Economics; au Economics, Geography na Mathematics; au Chemistry, Biology na Geography; au Physics, Chemistry na Biology; au Physics, Chemistry na Mathematics). Wanaotaka kujiunga wawe: wamezaliwa si kabla ya mwaka 1993; wamefaulu (A, B+, B, C au D) English na masomo yale yote waliyoyachagua; wamepata credits (A, B+, B au C) walau mbili katika masomo waliyoyachagua na ya tatu katika somo lolote walipofanya au waliporisiti mtihani wa kidato cha nne; wamepata credit ya tatu mwaka 2013 au 2014. Usaili utafanyika tarehe 13-6-2015 saa 2:00 asubuhi na utategemea vyeti (vya kuzaliwa, vya kuacha shule na hati za matokeo ya kidato cha nne). Washindi wataanza masomo tarehe 30-6-2015. Ada ni Tsh. 480,000 kwa mwaka. Kwa kukaa bweni wataongeza Tsh. 500,000. Jumla ni Tsh 980,000.

 

TUISHENI WAKATI WA LIKIZO (Civics, History, Geography, English, Kiswahili, Biology, Chemistry, Physics, Mathematics na Information & Computer Studies). Mpango huo mpya utaanza tarehe 1-12-2014 kwa wanafunzi wa shule yoyote ili kuwainua kitaaluma wakiwa likizo. Ada ni Tsh. 30,000 kwa mwezi. Kutakuwa na malipo ya nyongeza kwa mazoezi ya sayansi katika maabara.

 

 

MASOMO YA SEKONDARI KUANZIA ALASIRI (JUMAMOSI KUANZIA ASUBUHI)

Ni kwa wale watakaofanya mtihani wa maarifa (maarufu kama Q.T.) na mitihani mingine ya taifa kama watahiniwa wa kujitegemea. Bweni la wavulana halina nafasi kwa ajili yao.

 

P I: KUJIANDAA MIAKA MIWILI KWA MTIHANI WA MAARIFA (Civics, History, Geography, English, Kiswahili, Biology na Mathematics). Masomo yataanza tarehe 13-1-2015. Ada ni Tsh. 240,000 kwa mwaka. Kwa kukaa bweni wasichana wataongeza Tsh. 500,000. Jumla ni Tsh 740,000.

 

I-II: KUJIANDAA MWAKA MMOJA KWA MTIHANI WA MAARIFA (Civics, History, Geography, English na Kiswahili). Masomo yataanza tarehe 13-1-2015. Ada ni Tsh. 240,000 kwa mwaka. Kwa kukaa bweni wasichana wataongeza Tsh. 500,000, jumla ni Tsh 740,000.

 

P II: KUJIANDAA MWAKA MMOJA TENA KWA MTIHANI WA MAARIFA (Civics, History, Geography, English, Kiswahili, Biology na Mathematics). Wanaotaka kujiunga wawe na elimu inayolingana walau na ile ya kidato cha kwanza. Masomo yataanza tarehe 13-1-2015. Ada ni Tsh. 240,000 kwa mwaka. Kwa kukaa bweni wasichana wataongeza Tsh. 500,000. Jumla ni Tsh 740,000.

 

P III: KUJIANDAA MIAKA MIWILI TENA KWA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (Civics, History, Geography, English, Literature, Kiswahili, Biology na Mathematics; au Civics, History, Geography, English, Literature, Kiswahili na Information & Computer Studies). Wanaotaka kujiunga wawe na elimu inayolingana walau na ile ya kidato cha pili. Masomo yataanza tarehe 13-1-2015. Ada ni Tsh. 240,000 kwa mwaka. Kwa kukaa bweni wasichana wataongeza Tsh. 500,000. Jumla ni Tsh 740,000.

 

III-IV: KUJIANDAA MWAKA MMOJA KWA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (Civics, History, Geography, English na Kiswahili). Wanaotaka kujiunga wawe wamefaulu mtihani wa maarifa. Masomo yataanza tarehe 13-1-2015. Ada ni Tsh. 240,000 kwa mwaka. Kwa kukaa bweni wasichana wataongeza Tsh. 500,000. Jumla ni Tsh 740,000.

 

P IV: KUJIANDAA MWAKA MMOJA TENA KWA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (Civics, History, Geography, English, Kiswahili, Biology na Mathematics; au Civics, History, Geography, English, Literature, Kiswahili na Information & Computer Studies). Wanaotaka kujiunga wawe na elimu inayolingana walau na ile ya kidato cha tatu na wawe wamefaulu mtihani wa maarifa. Si watu wa kurisiti ule wa kidato cha nne. Masomo yataanza tarehe 13-1-2015. Ada ni Tsh. 240,000 kwa mwaka. Kwa kukaa bweni wasichana wataongeza Tsh. 500,000. Jumla ni Tsh 740,000.

 

T (= TARATIBU): KUJIANDAA MIAKA MIWILI KURISITI MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (Civics, History, Geography, English, Kiswahili, Biology na Mathematics; au Civics, History, Geography, English na Kiswahili). Wanaotaka kujiunga wawe wameshafanya ule wa kidato cha nne. Masomo yataanza tarehe 13-1-2015. Ada ni Tsh. 240,000 kwa mwaka. Kwa kukaa bweni wasichana wataongeza Tsh. 500,000. Jumla ni Tsh 740,000.

 

H (= HARAKA): KUJIANDAA MWAKA MMOJA KURISITI MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (Civics, History, Geography, English na Kiswahili) wawe wamepata credit (A, B+, B au C) walau moja katika somo lolote walipofanya au kurisiti mtihani wa kidato cha nne. Masomo yataanza tarehe 13-1-2015. Ada ni Tsh. 240,000 kwa mwaka. Kwa kukaa bweni wasichana wataongeza Tsh. 500,000. Jumla ni Tsh 740,000.

 

V-VI: KUJIANDAA MWAKA MZIMA KWA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA (History, Kiswahili na Language; au History, Geography na Kiswahili). Wanaotaka kujiunga wawe wamepata credits (A, B au C) walau tatu katika masomo yoyote walipofanya au waliporisiti mtihani wa kidato cha nne. Wawe pia wamepata walau D katika somo la English. Masomo yataanza tarehe 3-6-2015. Ada ni Tsh. 400,000 kwa mwaka. Kwa kukaa bweni wasichana wataongeza Tsh. 580,000. Jumla ni Tsh 980,000.

 

MAELEZO MUHIMU KWA WOTE

Ø Wakristo wa madhehebu yote wanatakiwa kusoma pia Bible Knowledge au Divinity; kwa wengine ni hiari.

Ø Ili kukwepa utapeli na ulanguzi, fomu za kujiunga zinapatikana hapa tu kwa Tsh. 20,000 na zinaweza kununuliwa hata siku ya usaili, mradi mhusika alete picha yake ya hivi karibuni au vielelezo vyote vinavyotakiwa.

Ø Inawezekana pia kupakua fomu kutoka tovuti ya shule halafu kulipa shuleni Tsh. 20,000 kwa kuigonga mhuri unayoihalalisha. Usikubali fomu bila mhuri.

Ø Mbali na fomu, malipo yoyote yanatolewa risiti katika ofisi ya mhasibu; nje ya hapo malipo si halali, na shule haihusiki nayo, hata kama aliyepewa pesa ni mwalimu. Jihadhari sana.

Ø Ada zote za bweni na zile za masomo ya asubuhi zinaweza kulipwa kwa mikupuo minne, lakini zile za masomo ya mchana zinatakiwa kulipwa kwa mkupuo mmoja; zaidi ya ada hakuna mchango unaodaiwa na shule.

Taaluma inadai idadi ya wanafunzi darasani isizidi kiwango fulani, kumbe msongo wa wanaotaka kusoma kwetu ni mkubwa mno: ndiyo sababu ni lazima tuwachuje sana. Kudai kupokelewa nje ya taratibu zilizopangwa ni kuwadhuru kielimu waliokwishaku