LITTLE BROTHERS & SISTERS OF  AFRICA

KISWAHILI ENGLISH ITALIANO ESPANOL

 

                                   

UNWA
Info
DIVINITY NOTES.BY BRO. RIKARDO MARIA, UNWA(2012 EDITION)
Stralci dalle Circolari (Raccolti dal compianto Enrico Riccioni)
Circolare 55

Ndugu Wadogo wa Afrika ni wanaume na wanawake Wafransisko wamisionari wa Kanisa Katoliki wenye makao makuu mjini Morogoro (Tanzania).

Cha kwao ni chama cha maisha yaliyowekwa wakfu kwa Mungu kwa njia ya ahadi ya kushika mashauri ya Kiinjili ya useja mtakatifu, ufukara na utiifu kadiri ya utamadunisho safi wa karama ya udugu na udogo waliyorithi kwa mtakatifu Fransisko wa Asizi.

Mtindo wa maisha yao unakusudiwa kumfuata Yesu kwa kutekeleza kijumuia Injili yake na kushikamana na watu wa leo walio fukara zaidi ili uwe habari njema kwao na kwa wale wote wanaotamani dunia ijae haki, amani na upendo.

Wakiamini kwamba hiyo itabaki ndoto ya mchana tu ikiwa wanaume na wanawake watajaribu kuujenga kwa nguvu zao wenyewe, Ndugu Wadogo wa Afrika wanaikimbilia sala usiku na mchana kusudi uhusiano na maongezi na Baba wa wote vizijalie akili furaha ya ukweli, viunganishe mioyo, vitakase na kuimarisha ndani ya kila mmoja nia ya kutumikia kwa ukarimu wenye shida kubwa zaidi na viwafanye wote kuwa vyombo vya amani yake.

Roho Mtakatifu, tunayeshirikishwa kwa njia ya Yesu mteswa, mzikwa na mfufuka, ndiye anayegeuza hivyo kila mmoja na wote kwa jumla ili kuwafanya kwa pamoja mashahidi wa Kristo hadi mipaka ya mwisho ya dunia.

Tangazo la jina lake, la maisha yake, la msalaba wake mtukufu, la fumbo lake na la mafundisho yake ndiyo huduma kuu wanayoweza kuwapatia ndugu zao katika ubinadamu.

Hilo linaendana na mipango ya kuendeleza watu na vitendo vidogovidogo vya kila siku ambavyo wanawashirikisha waliyojaliwa na mikono ya Mungu kwa njia ya kazi zao au kwa misaada ya watu wengine waliosogezwa jirani na utandawazi.

Ndugu Wadogo wa Afrika, wakijua kwamba wanachoweza kufanya ni kidogo kweli, wanatia maanani ushirika na viungo vyote vya familia ya Mungu, yaani Kanisa linaloongozwa na Papa na Maaskofu wenzake: ndani yake mchango wao mdogo kwa ustawi wa utawala wa Mungu unaweza kuwafaidisha wengi, kwa sababu upendo unazidishwa na uenezi wake.

Upendo huo unatakiwa kupamba kama moto ili kufuta aina yoyote ya ubinafsi na umimi inayowafunga watu ndani yao wenyewe na ya faida zao, ikiwafanya sio tu wasiweze kuzaa lolote bali waharibu maisha yao na ya wenzao, unavyothibitisha utamaduni wa Magharibi ambao umegeuka utamaduni wa kifo.

Kinyume chake, wao wanataka kudumisha, kustawisha na kueneza tunu bora za makabila ya Afrika ili wachangie utamaduni wa uhai na wa mshikamano usio na mipaka.

Ni kwa Maria, mama wa Yesu, kwamba wanataka kujifunza unyenyekevu wapokee neema ya moyo safi wenye kuwaka upendo ili kumshangilia Mungu na kumtumikia kila mtoto wake.  

The Little Brothers and Sisters of Africa are Franciscan missionaries of the Catholic Church based in Morogoro (Tanzania).

 

They form an association of life consecrated to God through the promise to observe the evangelical counsels of chastity, poverty and obedience according to a genuine enculturation of the charisma of fraternity and minority, which they have inherited from St. Francis of Assisi.

 

Their way of life aims at following Jesus through the fulfilment of his Gospel, all together and in solidarity with the most poor of the world today, so to become good news to them and to all people who hope for a world of justice, peace and love.

 

Believing that it will remain only a hopeless dream if men and women try to build it by themselves, the Little Brothers and Sisters of Africa pray day and night so that the assiduous contact and dialogue with the common Father may give to their minds the joy of his truth, unity of hearts, purity and strength in serving generously the most needy, and make them instruments of his peace.

 

It is the Holy Spirit, shared by Jesus dead and risen, who transforms anyone and everyone in such a way as to turn them into Christ’s witnesses up the last boundaries of the earth.

 

The proclamation of his name, his life, his glorious cross, his mystery and his teaching is the best service they can offer to their brothers and sisters in the world.

 

It is accompanied by works of human promotion and by little everyday deeds of sharing what they have received from God’s hand through their own work or contributions from people made nearby by the globalisation.

 

The Little Brothers and Sisters of Africa, knowing that what they can do is really something very little, value communion with all the members of God’s family, the Church guided by the Pope and his fellow Bishops: in unity with her, their little contribution for the building up of God’s kingdom can help many people by spreading love.

 

It is this love blazing like fire that eliminates any form of individualism and egotism which closes a person in himself and his profits, and so makes him not only sterile but also harmful to him and to others, as shown by today’s western culture, which has become a culture of death.

 

On the contrary, the Little Brothers and Sisters of Africa want to conserve, develop and diffuse the best values of the African peoples, in order to contribute to the establishment of a culture of life and solidarity at a global level.

 

It is from Jesus’ mother, Mary, that they want to learn humility, to be able to receive the gift of a pure heart burning with love, exulting in God and serving every child of God.

  

I Piccoli Fratelli e Sorelle d’Africa sono francescani missionari della Chiesa Cattolica con base in Morogoro (Tanzania).

La loro è un’associazione di vita consacrata a Dio tramite la promessa di osservare i consigli evangelici di castità, povertà ed obbedienza secondo una sana inculturazione del carisma di fraternità e minorità ereditato da san Francesco di Assisi.

La loro forma di vita si propone di seguire Gesù con la pratica comunitaria del suo Vangelo in solidarietà coi più poveri di oggi così da essere una buona notizia per essi e per tutti quelli che anelano ad un mondo di giustizia, pace ed amore.

Credendo che esso resterà solo un sogno se gli uomini e le donne cercheranno di costruirselo con le proprie forze, i Piccoli Fratelli e Sorelle d’Africa ricorrono alla preghiera giorno e notte perché l’assiduo contatto e colloquio col Padre comune doni alle menti la gioia della verità, unisca i cuori, purifichi e rafforzi in tutti l’intenzione di servire generosamente i più bisognosi, e ne faccia strumenti della sua pace.

E’ lo Spirito Santo, comunicato tramite Gesù morto e risorto, a compiere tale trasformazione di ognuno e di tutti per renderli insieme testimoni di Cristo fino agli estremi confini della terra.

L’annunzio del suo nome, della sua vita, della sua croce gloriosa, del suo mistero e del suo insegnamento costituisce il massimo servizio che possono rendere ai loro fratelli e sorelle in umanità.

Ad esso si affiancano opere di promozione umana e piccoli gesti quotidiani di condivisione di quanto ricevuto dalla mano di Dio attraverso il proprio lavoro o i contributi di gente resa vicina dalla globalizzazione.

I Piccoli Fratelli e Sorelle d’Africa, coscienti che quanto possono fare è veramente poco, valorizzano la comunione con tutti i membri della famiglia di Dio, la Chiesa guidata dal Papa e dai suoi colleghi Vescovi: in essa il loro piccolo contributo alla crescita del Regno di Dio può riuscire di vantaggio a tanti, perché l’amore diffondendosi si moltiplica.

E’ un amore che deve divampare come il fuoco per eliminare ogni forma di individualismo e di egoismo che chiude in sé stessi e nei propri interessi, rendendo non solo sterili ma dannosi a sé e agli altri, come dimostra la cultura occidentale divenuta una cultura di morte.

Al contrario, essi vogliono conservare, sviluppare e diffondere i migliori valori dei popoli africani per contribuire ad una cultura della vita e della solidarietà globale.

E’ da Maria, la madre di Gesù, che vogliono imparare l’umiltà per accogliere il dono di un cuore puro ed ardente di amore per esultare in Dio e servire ogni suo figlio.

 

Los Pequeños Hermanos y Hermanas de África son misioneros franciscanos de la Iglesia Católica con sede en Morogoro (Tanzania).


Esta es una asociación de vida consagrada a Dios a través de la promesa de observar los consejos evangélicos de castidad, pobreza y obediencia en función de una verdadera inculturación del carisma de fraternidad y minoridad que han heredado de San Francisco de Asís.


Su forma de vida tiene por objeto seguir a Jesús a través de la realización de su Evangelio, todos juntos y en solidaridad con los más pobres del mundo de hoy, a que pasen a ser una buena noticia para ellos y para todas las personas que tienen la esperanza de un mundo de justicia, la paz y la amor.


Convencidos de que seguirá siendo sólo un sueño sin esperanza, si los hombres y las mujeres tratan de construirlo por sí mismos, los Pequeños Hermanos y Hermanas de África oran día y noche para que el contacto y el diálogo asiduo con el Padre puede dar a su mente la alegría de su verdad, la unidad de corazones, la pureza y la fuerza en el servicio generoso a los más necesitados, y hacer que sean los instrumentos de su paz.


Es el Espíritu Santo, compartido por Jesús muerto y resucitado, que transforma a todos, de tal forma que se convierten en testigos de Cristo hasta los últimos límites de la tierra.


La proclamación de su nombre, su vida, su cruz gloriosa, su misterio y su enseñanza es el mejor servicio que pueden ofrecer a sus hermanos y hermanas en el mundo.


Va acompañada de obras de promoción humana y de a poco todos los días actos de compartir lo que han recibido de la mano de Dios a través de su propio trabajo o contribuciones de personas que cerca de la globalización.


Los Pequeños Hermanos y Hermanas de África, a sabiendas de que lo que pueden hacer es en realidad algo muy pequeño, el valor de comunión con todos los miembros de la familia de Dios (es decir, la Iglesia guiada por el Papa y los obispos a sus compañeros: en la unidad con ella, sus pocas contribuciones para la construcción del reino de Dios puede ayudar a muchas personas por la difusión de amor).


Es este amor ardiente como el fuego, que elimina toda forma de individualismo y el egoísmo que se cierra en sí mismo una persona y sus beneficios, y así lo hace no sólo estéril, sino también perjudicial para él y para otros, como lo demuestra la actual cultura occidental, que se ha convertido en una cultura de la muerte.


Por el contrario, los Pequeños Hermanos y Hermanas de África desean conservar, desarrollar y difundir los mejores valores de los pueblos africanos, a fin de contribuir a la creación de una cultura de la vida y la solidaridad a nivel mundial.


Es a partir de la madre de Jesús, María, que quieren aprender la humildad, para poder recibir el regalo de un puro corazón ardiente de amor, exultante en Dios y servir a todos los niños de Dios.